Thursday 11 February 2010

usilo lijua usiku wa kiza

day five.usilo lijua ni usiku wa kiza.msemo huu kawngu umekuja baada ya kupata faraja ktk taaluma niloipata kupitia somo la matumizi ya blogger.kiasi flani yamenipa mwangaza wa kuchati zaid ktk kujiendeleza ktk matumizi ya compuyuter kupitia kwenye internet'kawaida ya matumizi ya compuyuter yanahitaji uzalendo kwani ukiwa mwenye kuridhika na ulipo pata basi hutofaidika ila cha msingi ni kujiendeleza zaid kila siku kwa kutafuta vitu mbali mbali.ushauri wangu tuendelezwe zaid kitaaluma tulopata imesaidia lkn haijatutesheleza.asante sana.

Tuesday 9 February 2010

day two ukipenda

Nilicho jifunza siku ya mwanzo ni tofauti na siku ya pili.mwanzo ilikuwa ni kusikiliza zaid na kuangalia kwa upande wangu.lkn siku ya pili mafunzo kwangu yalianza kuwa mazuri baada ya kuelewa njia za matumizi ya internet ktk kutafuta habari mbali mbali duniani zikiwa za kiuchumi,kijamii,kisiasa na za kimaendeleo ndani na nje ya nchi ya tanzania.kwa kweli mafunzo haya kwangu mimi binafs nimeyafurahia kiasi cha kwamba nikimaliza hapa nitajiendeleza zaid kwa vile nimeona vitu vingi na vya muhimu ktk kujifunza na kufanya kazi ktk mazingira ya kitecnologia.pia ktk masomo nilosoma jana na leo nimependa somo la HOW INTERNET HAS CHANGED SOCIETIES’

Monday 8 February 2010

pemba ni kisiwa kilozungukwa na bahari na chenye mandhari nzuri ya rangi ya kijani.na wakaazi wengi wa kisiwa hicho ni wenye kujali utamaduni wao ikiwemo kuvaa mavazi ya kizanzibari kwani asilimia 99 ya watu wa pemba ni waislam'lkn pamoja na hayo ni wakarimu kwa wenyeji na wageni hasa ktk suala zima la usalama wa mali na makaazii.wananchi wa pemba wengi wao ni wafanya biashara ambao wako sehemu mbali ya tanzania'

pemba